Dully ataja idadi ya kolabo zake na Diamond Platunmz | Bepari Classic
Breaking News
Loading...

Alhamisi, 13 Oktoba 2016

Dully ataja idadi ya kolabo zake na Diamond Platunmz

Msanii wa muziki, Dully Sykes amesema mpaka sasa ana nyimbo sita ndani ambazo amemshirikisha Diamond Platnumz lakini hafikirii kuziachia.dully-sykes-ft-diamond-platnumz
dully-sykes-ft-diamond-platnumz
Muimbaji huyo ambaye anafanya vizuri na wimbo ‘Inde’ akiwa amemshirikisha ‘Harmonize’ wa WCB, amekiambia kipindi cha Planet Bongo cha EA Radio kuwa kwa sasa atakuwa anakwenda na mwendo wa kutoa kolabo tu.
“Sipo WCB Wasafi na wala sijasaini wasafi ila nipo nao karibu na nafanya kazi nao karibu, mpaka sasa nimefanya kazi zaidi ya sita na Diamond Platnumz na sifikirii kama zitatoka saizi,” alisema Dully Skyes
Pia muimbaji huyo ambaye pia ni mtayarishaji wa muziki, amesema kwa sasa ameanza maandalizi ya kazi yake mpya ambayo pia amedai ni kolabo.
Download Video and Put Comment
Toa Maoni Hapa Chini

google+

linkedin

0 comments:

POST A COMMENT