Hatma ya ukodishwaji Yanga Oktoba 23 | Bepari Classic
Breaking News
Loading...

Jumatano, 12 Oktoba 2016

Hatma ya ukodishwaji Yanga Oktoba 23

Dar es Salaam. Wakati mjadala wa kukodishwa Yanga kwa miaka 10 ukishika kasi, uongozi wa klabu hiyo umesema uamuzi wa mwisho utatolewa  kwenye mkutano mkuu wa Oktoba 23.

Katibu wa Yanga, Baraka Deusdedit amesema mkutano mkuu wa Oktoba 23 ndiyo utaamua hatima ya kukodishwa kwa klabu hiyo au la.

“Ajenda ya kukodisha klabu itapitishwa na mkutano mkuu ujao, akidi ikitimia kwa mujibu wa katiba yetu zoezi hilo litafanyika,” alisema Baraka na kufafanua.

“Yanga ‘inadili’ na wanachama wanaolipia kadi zao, wapo wenye kadi, lakini hawazilipii hao siwezi kuwazungumzia kwa sababu si wanachama hai.

“Ukizungumzia wanachama wa Yanga kiukweli ni wengi, ni zaidi ya 10,000, lakini wote hao si ‘active’ (hai).

Katibu huyo alisema mkutano mkuu wa dharura uliopita ulikuwa na wanachama 1,800 wanaolipia ada ya kadi zao za uanachama.

“Mambo mengine ni ya kiofisi, hayapaswi kutangazwa, lakini mkutano wetu mkuu wa dharura uliopita ulikuwa na wanachama 1,800 waliokuwa hai,” aliongeza Baraka.
Download Video and Put Comment
Toa Maoni Hapa Chini

google+

linkedin

0 comments:

POST A COMMENT